Polisi wa Chalinze, Pwani wamekamata Wahamiaji haramu 51 wa kiume eneo la Msata wakiwa wanasafirishwa leo August 22,2020.
"Polisi eneo la mizani Msata walilitilia shaka Lori na kulisimamisha, liliposimama Dereva na Konda wakajishtukia na kukimbia na kuliacha gari, tulipokagua mlango wa nyuma wamepanga madumu tupu ili kuwaficha, ukikagua haraka unaweza kudhani ni mafuta tu na ukawaruhusu ila tulipokagua zaidi tukaona kundi kubwa la Watu" - POLISI
Kwa sasa Wahamiaji hao wapo Kituo cha Polisi Chalinze kwa hatua za kuwakabidhi uhamiaji ili waendelee na taratibu nyingine za kisheria.
الفئة
عرض المزيد
تعليقات - 0
مقاطع الفيديو ذات الصلة على WAHAMIAJI HARAMU WANASWA MSATA: