المدة الزمنية 8:22

Jionee Ziara ya Waziri wa Ulinzi na JKT Alipotembelea Kamandi ya NAVY

بواسطة Ulinzi Channel
117 817 مشاهدة
0
462
تم نشره في 2021/10/14

Tarehe 12 Oktoba, 2021 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) amefanya ziara ya kutembelea Kamandi ya Jeshi la Wanamaji (Navy Command) iliyopo eneo la Kigamboni jijini Dar es Salaam. Mheshimiwa Waziri ametembelea Kamandi ya Jeshi la Wanamaji ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kutembelea Kamandi za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania MKOANI Dar es Salaam, kwa lengo la kujitambulisha, kujionea utayari kiutendaji, miundo pamoja na changamoto na namna wanavyokabiliana nazo kiutendaji katika kulinda mipaka ya nchi yetu kwa upande wa baharini na kwenye maziwa. Alipowasili Makao Makuu ya Kamandi hiyo alipokelewa na mwenyeji wake amabye pia, ni Mkuu wa Kamandi hiyo, Meja Jenerali Michael Mwanandenje Mumanga akiwa pamoja na wanadhimu wa Kamandi, Wakuu wa Vikosi na Shule pamoja na maafisa. Mara tu baada ya kuwasili Makao Makuu ya Kamandi, Mheshimiwa Waziri alipokea Salaam ya Heshima iliyoandaliwa na Gadi ya Mapokezi na kisha kusaini Kitabu cha Wageni, kabla ya kutembelea gati (dockyard) na chelezo (slipway) na ujenzi wa Jengo la Wodi ya Mama na Mtoto unaotekelezwa na Kamandi hiyo kwa kutumia fedha za ndani. Jengo hilo litapokamilika litakuwa limegharimu takribani milioni 120 na pia, litatoa huduma za matibabu kwa familia za Maafisa, Askari, Watumishi wa Umma pamoja na wananchi waishio maeneo ya jirani. Baada ya Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax kupatiwa Taarifa ya Utendaji ya Kamandi ya Jeshi la Wanamaji, iliyosomwa kwake na Meja Jenerali Mmanga, Taarifa iliyohusu Historia, Mkao wa Kamandi, Majukumu ya Kamandi, Maeneo ya Uwajibikaji, , Changamoto ya Miundombinu Zana na Vifaa, Mkakati wa Kamandi pamoja na Mapendekezo ya Kamandi ya kukabiliana na changamoto ziliyowasilishwa kwake. Akitoa taarifa ya Kamandi Jenerali Mmanga alimweleza Mhe Waziri kuwa, Kamandi ya Jeshi la Wanamaji ikiwa ni sehemu ya JWTZ, yenye majukumu makuu mawili. Majukumu hayo ni yale ya kiasili (Traditional Roles) yanayojumuisha kuimarisha ulinzi wa mipaka ya baharini na kwenye maziwa, operesheni zote ndani na nje, kusindikizaa meli za Biashara za hapa nchini na za nchi rafiki, kutoa misaada ya utaftuataji, uokoaji na uopoaji wa watu na vifaa kutoa misaada wakati wa maafa na majanga kwa kushirikiana na vikundi vingine, kufanya shughuli za kidiplomasia kwa meli zetu kutembelea mataifa mengine pamoja na kulinda raslimali za nchi yetu zinazopatikana baharini. Aidha, Meja Jenerali Mumanga alibaianisha aina ya pili kuwa ni yale majukumu ya kupambano dhidi ya uhalifu baharini na kwenye maziwa (Contemporary maritime Roles) yanayojumuisha utekaji na uporaji, ugaidi baharini, biashara za magendo, uvuvi haramu uchafuzi wa bahari, usafirishaji na usambazaji wa madawa ya kulevya pamoja na uhamiaji haramu. Mara tu baada ya kupewa taarifa hiyo, Dkt. Stergomena Lawrence Tax alimshukuru Mkuu wa Kamandi na Maafisa Wanadhimu kwa mapokezi mazuri aliyoyapata baada ya kuwasili hapo Makao Makuu ya Kamandi pamoja na taarifa nzuri iliyompa mwanga katika kutekeleza majukumu yake ndani ya Wizara. Aidha, Mheshimiwa Waziri aliweka bayana kuhusu madhumuni ya ziara yake kwenye Kamandi hiyo, kuwa ililenga kuwatembelea kwa lengo la kujitambulisha, kufahamiana, kujifunza shughuli mbalimbali wanazozifanya pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo. Na kupitia mhadhara huo, ameweza kujifunza mengi. Kuhusu changamoto, Mheshimiwa Stergomena Lawrence Tax amewaasa Wanamaji kuwa changamoto ni nyingi na ni halisi, cha msingi ni kuzifanyia uchambuzi wa kina kuona ni zipi ziweze kuchukuliwa hatua na Wizara kwa kuzingatia vipaumbele na zile changamoto ndogondogo ambazo ziko ndani ya uwezo wao waendelee kuzifanyia kazi. Mwisho Mheshimiwa Waziri aliwataka kuendelea kutekekeleza majukumu yao kwa weledi, maana Jeshi ni watu wanaofanya kazi kwa weledi.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 38