المدة الزمنية 6:51

MATUMIZI YA SALA YA BWANA KATIKA MAOMBI

بواسطة SIRI ZA BIBLIA
13 281 مشاهدة
0
182
تم نشره في 2021/05/20

#Mungu#Maombi#Wokovu#Biblia#Mathayo Mathayo 6;9-13 Yesu Kristo alipowafundisha wanafunzi wake kuomba aliwaelekeza kuomba kwa misingi inayojulikana kama sala ya Bwana, kimsingi hakuwa anamaanisha waitamke kama ilivyo na kuimaliza kama kasuku kama watu wengi wanavyofikiri , Biblia inaposema katika Mathayo 6;9 “Basi ninyi salini hivi baba yetu uliye mbinguni……” Tafasiri ya kiingereza ya King James Version inasema “After this manner therefore pray Ye” tafasiri ya kiingereza ya LIVING BIBLE inasema Pray alon these lines” Katika Luka 11;2 kwa msingi huo kinachozungumzwa hapa ni kuwa sala ya bwana ni mafundisho ya msingi ya kutumia katika maombi, kilichozungumzwa ni kuomba kupitia misingi hii kila tunapotaka kuomba Luka 9;54 Mathayo 20;20-22 Kutamka sala ya bwana kama ilivyo ingeweza kuchukua dakika mbili tu na isingelikuwa suluhisho la kufundisha maombi ambao wao walikuwa wakitaka kujifunza kuomba kwa muda mwingi wa kutosha kama alivyokuwa akiomba Bwana Yesu vinginevyo Yesu hangeshangazwa na wanafunzi wake kulala usingizi ikiwa sala Yenyewe ingeweza kuchukua dakika chache. Mafundisho mengi aliyokuwa akiyatoa Bwana Yesu Mara nyingi yalikuwa yakihitaji ufafanuzi Mathayo 13;36, na pia mafundisho ambayo wanafunzi waliweza kuyaelewa leo yanahitaji ufafanuzi Mathayo 13;51 Mengine ambayo yalikuwa magumu kueleweka kwa wanafunzi kwa mfano habari za kuteseka kufa na kufufuka sio tatizo kubwa kueleweka leo Marko 9;30-32, Luka 24;44-45 na ndio maana kanisa linahitaji waalimu ambao wanaweza kufunuliwa na Roho wa Mungu Neno lake ili kulilisha kanisa 1Wakoritho 2;10. JINSI YA KUOMBA KWA KUTUMIA SALA YA BWANA. Baba yetu uliye mbinguni.Mathayo 6;9. Tunapokuja kumuomba Mungu inatupasa kufahamu kuwa Yeye ni baba yetu, kama unaweza kuwasiliana na baba yako wa duniani anayejishughulisha na na mahitaji yetu na kuyajali ni muhimu kufahamu kuwa Hatupaswi kumuomba Mungu tukidhani kuwa yuko mbali ni lazima tuweke mawazo yetu kuwa Mungu ni baba yetu na kuwa yuko karibu mno tunapomuomba Zaburi 145;18,Zaburi 119;151 103;13 Fahamu kuwa ni baba mwenye upendo mwenye uwezo anayejishughulisha sana na mambo yetu 1Petro 5;6-7 hatupaswi kufikiri kuwa yeye hatujali Zaburi 37;28 Isaya 49;14-16,1Wakoritho 10;10. Aidha uhusiano wetu na Mungu lazima uwe wa baba na mwana maana yake kama hujazaliwa mara ya Pili huwezi kuwa na uhusiano wa aina hiyo.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 20