Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip
Mpango leo tarehe 21 desemba 2021 amekutana na kufanya
mazungumzo na viongozi wakuu wa kanisa la Wabaptist Tanzania
wakiongozwa na Askofu Mkuu Anorld Manase Molel, mazungumzo
yaliofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
Katika mazungumzo hayo Makamu wa Rais amewashukuru viongozi
pamoja na waumini wote wa kanisa hilo kwa kuendelea kuliombea taifa
katika kudumisha amani, umoja na mshikamano. Amesema jamii yeyote
yenye maadili mema na uzalendo inatokana na mchango mkubwa
unaotolewa na viongozi wa dini hapa nchini.
Amesema kanisa la Baptist limekuwa na mchango mkubwa katika
kushirikiana na serikali kutoa huduma za kijamii ikiwemo elimu na afya
hivyo amewaasa viongozi hao kuendelea kutoa huduma hizo ikiwemo
kufungua upya chuo kikuu walichokuwa wanakimiliki hapo awali cha
Mount Meru.
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: https://www.facebook.com/Spotileo-176 ...
HabariLeo: https://www.facebook.com/habarileo/
DailyNews: https://www.facebook.com/dailynewstz/
INSTAGRAM;
HabariLeo: https://instagram.com/habarileo_tz?ig ...
SpotiLeo: https://instagram.com/spotileo?igshid ...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: https://twitter.com/HabariLeo?s=09