SOMO: NI KWA JINSI GANI WAWEZA KUKABILIANA NA VITA NA MADHARA YA MANENO YANAYOACHILIWA KUKABILIANA NA WEWE
NA: MCH. MARTHA RICHARD
Katika vita vya kiroho huwa yanatumika maneno
Sababu ya vita ya maneno ni ili kuharibu mtazamo au mwelekeo wa maisha yako. Hii huwa na lengo la kukuchafua
WAEBRANIA 4:12
maana neno la Mungu li hai…..tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho
UFUNUO 19:11-15
ZABURI 55:21
Kinywa chake ni laini kuliko siagi….Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Bali hayo ni panga wazi
MITHALI 26:28
ulimi unenao uongo huwachukia wale uliowajeruhi
AYUBU 5:21
Utafichwa na mapigo ya ulimi, wala usiogope maangamivu yatakapokuja
Note: huna namna ya kuzuia vita au maneno yanayokuja juu yako ila una namna ya kukabiliana nayo
ISAYA 54:17….
.kila ulimi utakao inuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa
MATENDO 28:3-5
Moyo wa mtu ni mzuri sana katika kukuza maneno yanayoingia kwani ni mahali ambapo maneno husitawi
Note: Sio kila neno litokalo kwa adui ni baya bali kuna neno la kuchukua kwa ajili ya kuendelea kwako.
MUHUBIRI 7:21
WAEFESO 6:16
Zaidi ya yote mkitwaa ngao ya Imani ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote ya yule mwovu
WAEBRANIA 11:33-34
Kwa Imani walishinda milki za wafalme…waliokoka na makali ya upanga
USIRUHUSU
1: Uchungu (WAEBRANIA 12:15)
2: Usiruhusu kuto kusamehe
3: Usiruhusu kisasi