Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mwita Waitara amechukizwa na vitendo vya wananchi wanaozunguka eneo la mradi wa ujenzi wa reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Isaka- Mwanza kituo cha Malampaka wilayani Maswa Mkoa wa Simiyu kuiba mafuta ya kuendeshea magari na mitambo ya mkandarasi anayetekeleza ujenzi huo.