Halmashauri ya Jiji la dodoma imeendelea kutatua kero na migogoro ya ardhi katika kata ya Nzuguni mtaa wa Kitelela kwa kuweka kambi ya siku saba katika eneo hilo
Zoezi hilo lilitolewa na mkurugenzi wa jiji la Dodoma Joseph Mafuru katika mkutano wa hadhara aliofanya katika mtaa huo wenye lengo la kusikiliza kero na migogoro iliojitokeza katika zoezi la upimaji ardhi uliofanyika katika eneo hilo
Akijibu na kutolea ufafanuzi baadhi ya changamoto zilizo jitokeza kwa wananchi katika zoezi la upimaji ikiwemo swala la asilimia 70% kwa mwananchi na asilimia 30% kwenda halmashauri ya jiji Mafuru aliwasisitizia kuwa maeneo ya miundombinu kwa ajili ya huduma za kijamii nimuhimu kuwepo katika kila eneo
hata hivyo mkurugenzi aliwaahidi wananchi hao kuweka kambi ya wataalamu wa ardhi mtaa huo kwa muda wa siku saba kwa lengo la kutatua migogoro na kulekebisha kasoro zilizo jitokeza katika zoezi la upimaji
الفئة
عرض المزيد
تعليقات - 2
مقاطع الفيديو ذات الصلة على Maafisa ardhi Jiji la dodoma kuweka kambi ya siku 7 katika kata ya Nzuguni mtaa wa Kitelela: